Header Ads


IGP SIMON SIRRO ALIPOTEMBELEA TANGA PRESS CLUB



ASKARI WAKIWA TAYARI KUMARIBISHA IGP


MWENYEKITI TANGA PRESS AKIMKARIBISHA MKUU WA JESHI LA POLISI WAKATI ALIPOTEMBELEA TPC





MWENYEKITI TANGA PRESS HASSAN HASHIM  AKITOA UTAMBULISHO 





MKUU WA JESHI LA POILISI AKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA WAANDISHI WA HABARI TANGA


Hassan Hashim Tanga.

Mkuu wa jeshi la Polisi nchini INSP Jen Simon Siro amewataka waandishi wa habari kutanguliza uzalendo kwa kuandika taarifa  zinazochochea maendeleo na kuondoa migogoro kwa wananchi

Kauli hiyo ameitoa  katika mkutano na vyombo vya habari uliofanyika katika ukumbi wa Tanga press club.

Amesema vyombo vya habari vinawajibu mkubwa wa kuibua fursa za kiuchumi badala ya kuandika habri za uchochezi

Akizungumzia ziara yake mkoani Tanga IGP Siro amesema imelenga kumbusha wajibu wa askari  katika utendaji kazi  na kujiepuka vitendo vinavyochafua sifa ya jeshi hilo.

Kuhusu masuala ya usalama mkuu huyo wa jeshi la polisi amesema kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama wataimarisha ulinzi katika mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Uganda hadi Tanga.

No comments:

Powered by Blogger.