Header Ads


King Majuto asikitishwa na uzushi wa mitandao ya kijamii

NA Hassan Hashim, Tanga.
King Majuto asikitishwa na uzushi wa mitandao ya kijamii

Msanii gwiji wa maigizo ya vichekesho  nchini Amri Athuman  (King Majuto) ametoa rai kwa watanzania kuwa makini katika matumizi ya mitandao ya kijamii ambayo kwa kiasi kikubwa imekua ikitumika vibaya na  kuleta madhara kwa  jamii.

Kauli hiyo ameitoa katika mahojiano maalum yaliyofanyika nyumbani kwake Donge kufuatia uvumi uliozagaa nchini kupitia mitandao ya kijamii kwamba amefariki dunia.

Amesema kitendo cha kusambaza habari za uzushi wa kumhusisha yeye kwamba amefariki zimeleta mshituko mkubwa na usumbufu kwa familia yake pamoja na marafiki na kuiomba serikali kuwadhibiti wanatumia vibaya mitandao ya kijamii.

Majuto amesema kitendo kuzushiwa kifo kimejirudia zaidi ya mara tano sasa hali inayoonesha kwamba huenda kuna watu ambao wanafanya hivyo kwa malengo maalum wanayoyajua wenyewe na kuongeza kuwa anawasiliana na mwanasheria wake ili kuchukua hatua stahiki. 


Akizungumzia hali yake kiafya Majuto amesema julai 15 mwaka huu alilazwa katika kituo binafis cha Tanga Health centre na kufanyiwa upasuaji  mdogo wa hernia na kuruhusiwa julai 18 ambapo  kwa sasa anaendelea na mazoezi madogo nyumbani kwake.

MWISHO


KING MAJUTO AKIWA NYUMBANI KWAKE 

HAPA AKIWA NA WATOTO WAKE  MTAA WA DONGE JIJINI TANGA



MWANDISHI  WA TANGAJAMII BLOG AKIWA NYUMBANI KWA MZEE MAJUTO

No comments:

Powered by Blogger.